KUMBUKUMBU
Kilichofanyika kwangu,
kimefunza hakika
Kuishi na walimwengu, ni utu
na kadhalika,
Yote tumuachie Mungu, yatosha
tulipofika,
Nina kumbukumbu nzuri, nina kumbukumbu mbaya.
Nikisha kusimulia, huruma
tanionea,
Majina utanipea, Kwa yale
nilopitia,
Nikweli sikusikia, ya baba
alonambia,
Nina kumbukumbu nzuri, nina
kumbukumbu mbaya.
Wema ulinitongea, nikajipata pabaya,
Kwa kweli sikudhania,
yatanitokea haya,
Amini nilikusaidia, yote
kumpatia,
Nina kumbukumbu nzuri, nina
kumbukumbu mbaya.
Hadithi, hadithi njoo…Lakini hutoamini,
Tuache hadithi hio, sijui
niseme nini,
Kidogo tena sikia, tuchambue
jaladani,
Nina kumbukumbu nzuri, nina
kumbukumbu mbaya.
Hua ni giza totoro, kile
usichokijua,
Hakuonyesha kasoro, pale
tulipoanzia,
Ningeina tumoro,Ruwa ningelikimbia,
Nina kumbukumbu nzuri, nina
kumbukumbu mbaya.
Nimetamani kuchora, yote
niloyapitia,
Yamejaa kwa fikira, yamejaa
kwa hisia,
Mengine yananikera, mengine
yanisumbua,
Nina kumbukumbu nzuri, nina
kumbukumbu mbaya.
Nitachora siku moja, iwe kama
ya filamu,
Kwa sasa, naomba, ngoja,
tuitayarishe hamu,
Ili tunapoitaja, iwe
tunaifahamu,
Nina kumbukumbu nzuri, nina
kumbukumbu mbaya.
Duizo nimezikwepa, nakiri
kutorudia,
Sirudii ninaapa, nitaishi
kungojea,
Mola wangu atanipa, heri sasa
kungojea
Nina kumbukumbu nzuri, nina
kumbukumbu mbaya.
Green Ruwa
Mtoto Wa Gwiji
No comments:
Post a Comment