CHAPATI ZA KUMI NAIROBI
Nairobi, mji mkuu nchini Kenya wenye watu takriban milioni 4.397 ambao asili mia 60% ya wakaazi hao ni wafanya biashara. Uuzaji wa chapati Nairobi umekuwa ukinawiri kifaida ndani na nnje ya mji, ila kinachowapa taabu wanunuzi ni ambapo chapati hizi zinapouuzwa bei ghali kinyume na matarajio yao.Kutokana na utafiti wa matumizi ya ngano, imebainika wazi kwamba katika kila mwaka ngano hutumika kwa asii mia 47% ikilinganishwa na vyakula vyengine hata kwa jinsi bei ya vyakula vya ngano kama chapati kuuzwa bei ghali.
Wanunuzi wengi wa chapati huwa vijana wanaofanya vibarua na wanabiashara wadogowadogo katika masoko na vituo vya mabasi, mara nyingi wateja wa chapati hupewa chakula hiki pamoja na mchuzi wa bure katika vibanda na hoteli nyingi zilizopo kando kando ya barabara na pia nnje ya maduka makbwa makubwa mjini Nairobi,
Iwapo mtu angetaka chapti za shilingi kumi basi ni vyema kuwa tayari kuingia katika soko kubwa mjini Nairobi, 'Muthurwa'. Katika soko hili chapati huuzwa kwa shilingi kumi, ni wachache wanaojua mahali ambapo chapati hizi za shiliingi kumi huuzwa. Julai 20.2021 niliweza kufika katika kibanda kimoja Muthurwa na kununua chapati ya shilingi kumi, hapa nilipakuliwa chapti hio kwa mchuzi wa maharagwe ambao uikuwa mchuzi wa bure. ''Hoteli hii hupata watu wasiopungua mia mbili kila siku'' alisema meneja wa hoteli hio. Kizuri zaidi katika hoteli hii ni kwamba mteja anaweza kulipa kupitia simu kwa mtandao wowoe ule.
Magharibi mwa soko hili la Mudhurwa ndipo hoteli kama hii ya chapati za shilingi kumi na vyakula vyengine vitamu vya bei ya chini hupatikana. Mara kwa mara upande huu wa soko hupaswi kuamini watu hususan kwa barabara. Ni vizuri kuwa na ufahamu kamili wa pale unapoelekea katika soko hili maana vijana waliokaa kandokando ya njia hizi huwa na njama za kuwapora wapita njia pasi kutaka kujua wakati au masaa ya siku .


